KAMANDA MAGOMI ATHIBITISHA KUKAMATWA KWA BABA ANAYETUHUMIWA KULAWITI WATOTO WAKE WA SHULE YA MSINGI KATIKA MANISPAA YA SHINYANGA

Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linachunguza tukio linalomhusisha mwanaume mmoja kwa tuhuma za kuwalawiti watoto wake wawili wanafunzi wa shule ya msingi Mapinduzi B, iliyopo kata ya Ngokolo Manispaa ya Shinyanga.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kamishna msaidizi wa Polisi Janeth Magomi amethibitisha mwanaume huyo kukamatwa kwa ajili ya uchunguzi.

Kamanda Magomi amesema upelelezi utakapokamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.

Akizungumzia tukio hilo kaimu mganga mfawidhi wa Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Dkt. Kambi Butete amesema Februari 22 Mwaka huu majira ya saa tano asubuhi watoto hao walifikishwa katika Hospitali hiyo na kufanyiwa uchunguzi wa kidaktari ambapo majibu ya vipimo vyao yamekabidhiwa kwa vyombo vya usalama kwa ajili ya hatua za kisheria.

Misalaba Blog imezungumza na  Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Mapinduzi B, Hassan Hemed ambaye ameeleza namna alivyopokea taarifa za tukio hilo, na kusema kuwa kushamiri kwa matukio hayo inachangiwa na wazazi na walezi kutowajibikia jukumu la malezi bora na makuzi kwa watoto.

‘Hizi taarifa za hawa watoto wawili nilizipokea kwa kuletewa na watu ambao wao wanasema ni wana harakati ndiyo waliniletea hawa watoto saa sita usiku asubuhi nikaenda kwa hawa watoto mpaka wanapoishi mpaka ndani kwako bi kweli wanalala chumba kimoja na baba yao mzazi’.amesema Mwalimu Hemed

Taarifa za kulawitiwa kwa watoto hao ziliripotiwa kwa Mwalimu mkuu wa shule ya Msingi Mapinduzi B, usiku wa Februari 22, Mwaka huu 2023.

TAZAMA VIDEO HAPA CHINI