Na Mapuli Misalaba, Shinyanga
Wakristo katika idara ya wanawake kanisa la AICT
Negezi lililopo kata ya Masekelo Manispaa ya Shinyanga wametakiwa kufanya
maombi ili mwenyezi Mungu aimarishe ndoa na kubariki familia zao.
Rai hiyo imetolewa leo na Mwinjilisti Queen Stephano
wa kanisa la Mtakatifu Yohana Ndala
wakati akihubiri kwenye ibada ya Jumapili iliyofanyika katika Kanisa la AICT
Negezi Manispaa ya Shinyanga Mkoani Shinyanga.
Amesema kuwa wanawake hawana budi kutumia muda wao
kufanya maombi kwaajili ya kuombea familia zao ili ziepukane na matendo yasiyompendeza
Mungu.
Mwinjilisti Queen amesema ni muhimu kila mwanamke
kutumia hekima na busara katika maisha yao ya kila siku pamoja na Ndoa bila
kusahau malezi bora kwa watoto ambayo
yatasaidia kuepusha mifarakano kwenye
familia na jamii kwa ujumla.
Aidha Mwinjilisti Queen ametumia fursa hiyo kuwakumbusha wakristo kujenga tabia ya
kuombeana wao kwa wao huku akiwasisitiza kuombea Taifa hasa vijana kuepukana na
mambo yasiyompendeza Mwenyezi Mungu kama vile Mapenzi ya jinsia moja ambayo yamekuwa ni
chukizo kwa jamii na Taifa kwa ujumla.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa idara ya wanawake na
watoto Kanisa la AICT Local Church ya Negezi Esther Joram amesema idara hiyo
imeamua kutumia siku ya leo kuhitimisha siku ya wanawake ambayo ilikuwa ikienda
sanjari na wiki ya akina mama wa Makanisa ya AICT.
Esther amewaomba wanawake wengine kuendelea kuimarisha
umoja wao na kwamba ameihidi kuendelea kutoa elimu kwa wanawake wengine ili
kuishi katika maisha yenye hekima na maarifa.
Baadhi ya wanawake katika idara ya wanawake Local
Church ya Negezi waliohudhuria kwenye ibada hiyo wamesema ushirikiano ni muhimu
ili kuimarisha nguvu ya maombi huku wakimpongeza Mwinjilisti Queen kwa mahubiri
yake mazuri.
Mwinjilisti Queen Stephano wa kanisa la Mtakatifu Yohana Ndala wakati akihubiri kwenye ibada ya Jumapili iliyofanyika katika Kanisa la AICT Negezi Manispaa ya Shinyanga Mkoani Shinyanga.
Social Plugin