Na Mapuli Misalaba, Shinyanga
Shirika lisilo la
kiserikali la Mkoani Shinyanga, Companion of Woman and Children Empowerment
(COWOCE) limewakumbusha wazazi na walezi kuhamasika na uchangiaji wa chakula
cha wanafunzi shuleni ili kuimarisha afya zao.
Akizungumza leo katika
zoezi la kuhamasisha wazazi kuchangia chakula cha wanafunzi shuleni Mkurugenzi wa shirika la COWOCE Bwana Joseph Ndatala
amesema ni muhimu wazazi kuchangia chakula shuleni ili kuwaepusha na magojwa
ikiwemo vidonda vya tumbo.
Mkurugenzi Ndatala wakati
akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari Ndala amewasisitiza wanafunzi
hao kwenda kuwaambia wazazi na walezi juu ya umuhimu wa kupata chakula shuleni.
“Utafiti unaonesha wazi kuwa mtoto ambaye
amekwenda shule ya awali anafanya vizuri sana shuleni lakini unaambatana na kuwa
mtoto anayekula shuleni anafanya vizuri sana darasani kuliko mtoto ambaye hali.
Kama mtoto anaingia darasani saa mbili asubuhi mpaka saa 11 jioni hajala kamwe
hawezi kumsikiliza vizuri mwalimu”,ameeleza Mkurugenzi Ndatala
“Tumekuja hapa tukiambatana na Vikundi vya
COWOCE A na B vinavyosimamiwa na shirika letu la COWOCE linalojihusisha na haki
za wanawake na watoto na kuwajengea uwezo wa kujiajiri vijana”.
“Lengo kubwa siyo kuja kutoa msaada bali lengo
kubwa sana ni kufikisha ujumbe kwa wazazi wenu na walezi wenu kwamba wana
wajibu wa kutoa chakula shuleni. Watoto wengine wapo kwenye mazingira magumu
lakini haiwezekani mnakosa hata 1,000/= au 4000/= ya chakula kwa mtoto”,amesema
Mkurugenzi Ndatala.
“Hakuna mtoto asiyekula chakula nyumbani, sasa
kama watoto wote tunakula chakula nyumbani usiku, naomba tupeleke ujumbe kwa
wazazi wachange chakula angalau kidogo kidogo ili muweze kusoma vizuri tupate
Mawaziri humu, Wabunge, Madiwani wanaotoka shule zetu kwa sababu chakula
kinaongeza afya. Ili tuwe na lishe bora lazima tule chakula”.
“Hapa
tumekuja na chakula kidogo ambacho kwa niaba yenu wanafunzi wachache watapokea
hicho chakulaIkiwa ni sehemu ya kuhamasisha utoaji wa chakula shuleni, wazazi
watoe chakula na nyinyi watoto msome shule. Pia tunampatia chakula (Mchele kilo
22) mwanafunzi mmoja wa shule ya Sekondari Masekelo kw ajili ya kula shuleni.
Hapa katika shule ya Sekondari Ndala tumeleta kilo 30 za mchele”,ameongeza
Mkurugenzi Ndatala.
Bwana Ndatala ambaye pia
ni Mwenyekiti wa wazazi katika shule hiyo ya Ndala sekondari, ametumia nafasi
hiyo pia kuwasihi wanafunzi kusoma kwa bidii ili kufikia malengo yao ambapo pia
amewasisitiza kujiepusha na vishawishi vibaya katika safari yao ya masomo.
Aidha shirika la COWOCE kwa
kushirikiana na Vikundi vya wanawake wanaojihusisha na ujasiriamali vilivyojengewa
uwezo na Shirika hilo wametoa msaada wa vyakula kilo 30 za mchele katika
shule ya sekondari Ndala pamoja na kukabidhi kilo 22 za mchele kwa mwanafunzi
wa shule ya sekondari Masekelo Vailet Christopha ambaye anaishi katika
mazingira magumu.
Wakizungumza kwa niamba
ya wanafunzi wa shule ya sekondari Ndala Alam Petro pamoja na Vailet Christopha
mwanafunzi wa shule ya sekondari Masekelo Manispaa ya Shinyanga wamelishukuru
shirika la COWOCE kwa kutoa msaada huo.
Awali akizungumza Mwenyekiti wa COWOCE A, Magdalena Yohana amewakumbusha
wanafunzi hao kumtumaini Mungu katika
maisha yao ya kila siku na kwamba wanapaswa kusoma kwa bidii huku
wakimtanguliza mwenyezi Mungu.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa COWOCE B, Mosi Rashid amewaomba
wazazi na walezi kuchangia chakula kwa wanafunzi shuleni ili kuongeza ufaulu
kwenye mitihani yao.
Naye Mjumbe wa COWOCE A, Happy Mathias amewasisitiza wanafunzi
kuacha kujiingiza kwenye masuala ya mapenzi kwani yanachangia mimba za utotoni
na kuathirika kwa magonjwa mbalimbali ikiwemo ugonjwa wa upungufu wa kinga
mwilini VVU na UKIMWI hivyo amewaomba kujiepusha nayo ili waweze kutimiza ndoto
zao.
Akizungumza kwa niamba ya Mkuu wa Shule ya Sekondari Ndala, mwalimu wa
taaluma katika shule hiyo Samweli James amesema ipo changamoto kwa baadhi ya
wanafunzi wanaotoka katika familia zenye mazingira magumu kushindwa kuchangia
chakula chao.
Mwenyekiti wa COWOCE A, Magdalena Yohana na Mwenyekiti wa COWOCE B, Mosi Rashid wakimkabidhi
msaada wa chakula kilo 22 za mchele mwanafunzi wa shule ya sekondari Masekelo
Vailet Christopha.
Mwenyekiti wa COWOCE A, Magdalena Yohana na Mwenyekiti wa COWOCE B, Mosi Rashid wakimkabidhi
msaada wa chakula kilo 22 za mchele mwanafunzi wa shule ya sekondari Masekelo
Vailet Christopha.
Mwenyekiti wa COWOCE A, Magdalena Yohana na Mwenyekiti wa COWOCE B, Mosi Rashid wakimkabidhi
msaada wa chakula kilo 22 za mchele mwanafunzi wa shule ya sekondari Masekelo
Vailet Christopha.
Vailet Christopha
mwanafunzi wa shule ya sekondari Masekelo Manispaa ya Shinyanga akilishukuru
shirika la COWOCE kwa kutoa msaada huo.
Social Plugin