Na Mapuli Misalaba, Shinyanga
Wananchi na watumiaji wa Barabara ya Uhuru kipande cha Lubaga
Old-Shinyanga wameiomba TANROAD Mkoa
waShinyanga kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo ili kuondoa usumbufu kwa
watumiaji.
Wamesema ni takribani miezi minne tangu kuanza kwa ujenzi wa barabara
hiyo lakini imeshindwa kukamilika huku vifusi vilivyomwagwa vikisababisha
usumbufu kwa watumiaji ikiwemo ajali na vumbi linalotishia usalama wa afya za
wakazi wa maeneo hayo.
Wamesema kutokamilika kwa wakati kwa barabara hiyo inaathiri biashara
zinazofanyika kandokando ya barabara hiyo yakiwemo maduka na shughuli za mama
lishe ambao wamedai mazingira hayo yamewakosesha wateja.
Wameishauri serikali kutoa tenda kwa wakandarasi wenye uwezo na vifaa
vinavyotosha kutekeleza miradi hali ambayo itasaidia kukamilika kwa wakati kwa
ujenzi wa miundombinu.
Mmoja wa wenyeviti wa serikali za mitaa Bwana Philemon Chikala wa mtaa wa majengo mapya
moja ya maeneo unapofanyika uboreshaji wa miundombinu ya barabara ambaye
amesema utekelezaji wa miradi hauwashirikishi viongozi wa eneo husika.
Misalaba Blog imezungumza na
meneja wa mamlaka ya udhibiti wa barabara TANROADS Mkoa wa Shinyanga Mhandisi
Mibara Ndirimbi ametaja baadhi ya changamoto zinazokwamisha kukamilika kwa
mradi huo ambapo pia amewaomba wananchi kuwa wavumilivu wakati huo ambapo
juhudi za kukamilisha mradi huo zinaendelea.
“Mradi ule ulianza mwishoni mwa mwezi wa kumi
na unatarajia kukamilika mwezi wa sita lakini mradi huo hatutarajii kumalizika
mwezi wa sita tunatarajia utakamilika mwanzoni mwa mwezi wa nne”
“Changamoto ambayo ilikuwa ikichelewesha ni
kwamba uzalishaji wa ile CRR inatoka nje ya Mkoa na kule ambako inazalishwa
kulikuwa na changamoto ya uzalishwaji yale matirio na hiyo mkandarasi alikuwa
akitueleza mara kwa mara”.amesema
mhandisi Ndirimbi
Social Plugin