
Wakazi wa Mtaa wa Magadula
Kata ya Ngokolo katika Manispaa ya Shinyanga wameomba Wakala wa Barabara Mjini
na Vijijini TARURA kutekeleza kwa kiwango chenye ubora miradi ya maendeleo
ikiwemo miundombinu ya barabara.
Wameyasema hayo kwenye
mkutano wa hadhara uliofanyika juzi ambapo pamoja na mambo mengine wananchi hao
walibainisha baadhi ya kero ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya barabara
isiyokidhi kiwango cha ubora.
Wananchi hao pia
wamesema usafi wa mazingira ni jambo linalohitaji juhudi za pamoja na wengine
wakalalamikia ufugaji holela unaochangia uharibifu wa mazingira.
Kwa upande wake
Mwenyekiti wa Mtaa huo Bwana Humphrey Mtafungwa ameahidi kuchukua hatua za
haraka kushughulikia kero zote zilizopo katika mtaa huo kwa kuwashirikisha
TARURA, Ofisi ya Mazingira pamoja na Ofisi ya Afisa Mifugo.
Akisoma taarifa ya
utekelezaji wa shughuli za maendeleo Kaimu Mtendaji wa Mtaa wa Magadula Bwana
Joshua Marco amesema serikali ya mtaa huo imeendelea kutoa elimu ya uraia kwa
wananchi kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo ushiriki wa wananchi katika kuzuia
uhalifu na wahalifu ambapo pia ameagiza kuzingatiwa kwa usafi wa mazingira.
Mwenyekiti wa mtaa wa Magadula
Humphrey Mtafungwa amefanya mkutano wa
hadhara kwa lengo la kusikiliza kero na changamoto za wananchi zilizopo katika
mtaa huo.
Social Plugin