Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga
Mh. Johari Mussa Samizi amewataka wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji wa
madini kufanya kazi hiyo kwa utashi na kujituma ili kuchochea ukuaji wa uchumi
imara kupitia sekta hiyo.
Ameyasema hayo wakati akifungua
kongamano la wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji madini mbalimbali kanda
ya ziwa ikiwemo gesi asilia na mafuta ambalo limeandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali ambapo DC Samizi amewapongeza wanawake wanaofanya shughuli za madini.
Amesisitiza kuwa ni muhimu wananchi hasa wanawake
kuendelea kupewa elimu sahihi ya
uchimbani madini kupitia njia mbalimbali ikiwemo kufanya mikutano ya hadhara
ili waweze kuimarika na kufikia malengo yao.
Dc Samizi amevitaka
vikundi vya wanawake wachimbaji wa madini kutumia maadhimisho ya siku ya
wanawake Duniani kufanya mabadiliko ya kifikra na kiutendaji kutoka hatua moja
kwenda hatua nyingine zaidi.
“Tufanye
kazi yetu akina mama kwa moyo wote na kwa maarifa yote ili shughuli yako isiwe
palepale ulipodhani ipande kama ndoto zako zinavyofikiria kwamba siku moja na
mimi nitafika pale kwa wale ambao waliogopa kuthubutu mimi nawaambia mthubutu”.
“Nitumie
pia fursa hii kupitia jukwaa hili kuwatakia
kheri ya siku ya wanawake wanawake wote wa nguvu na shupavu wote mliopo humu
ambao mnapambana na sekta ya madini lakini niwakumbushe tu kwamba usiwe mwezi
wa kupendeza, kupaka mekapu, kupaka wanja na poda uwe mwezi wa kubadilika
kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine”.amesema DC Samizi
Mkuu huyo wa Wilaya
amezitaka taasisi zinazosimamia wachimbaji wa madini ikiwemo tume ya madini
pamoja na taasisi ya hakiRasilimali kuendelea kuyaelimisha makundi hayo kuhusu
uchimbaji bora na athari zake.
“Waliopewa
jukumu la kusimamia sekta ya madini wahakikishe kwamba wanasimamia sheria, kanuni
na taratibu zinazoongoza na zinazoelekeza namna gani ya kuitekeleza Local
Content kwa sababu ikitekeklezwa inavyohitajika yale malalamiko ya aki mama
sidhani kama tutayasikia tena na kama tutayasikia basi kidogosana”.amesema
DC Samizi
Kwa upande wake mtafiti
na mchambuzi wa sera kutoka taasisi ya Haki-Rasilimali Bwana Paul Mikongoti ameiomba
serikali kuweka msukumo katika ufuatiliaji na usimamizi wa sera na sheria
zilizotungwa kusimamia sekta ya madini.
“Tumeshatunga
sheria nzuri ambazo zinasimamia sekta yetu na hizo sheria tumeanza kuzitunga
toka siku nyingi na tumeziboresha mara nyingi sasa ni wakati wa kuhakikisha
kwamba hizi sera na sheria zinatekelezwa kwahiyo turudi tuweke nguvu katika
utekelezaji serikali iwe na mkono mrefu katika ufuatiliaji”.amesema
Bwana Mikongoti
Baadhi ya wanawake wamempongeza mkuu wa Wilaya ya Shinyanga ambapo wameahidi
kuendelee kufanya kazi kwa bidii ili waweze kufikia malengo yao.
Kongamano la Haki-
Rasilimali limefanyika mjini Shinyanga llikijumuisha wadau mbalimbali wa sekta
ya madini, ikiwemo vikundi vya wanawake wachimbaji wa madini, wataalam kutoka
tume na wizara ya madini ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya wanawake
Duniani.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mh. Johari Samizi akizungumza kwenye kongamano la wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji madini mbalimbali kanda ya ziwa ikiwemo gesi asilia na mafuta ambalo limeandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali.
kongamano la wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji madini mbalimbali kanda ya ziwa ikiwemo gesi asilia na mafuta ambalo limeandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali, likiendelea mjini Shinyanga
kongamano la wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji madini mbalimbali kanda ya ziwa ikiwemo gesi asilia na mafuta ambalo limeandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali, likiendelea mjini Shinyanga
kongamano la wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji madini mbalimbali kanda ya ziwa ikiwemo gesi asilia na mafuta ambalo limeandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali, likiendelea mjini Shinyanga
kongamano la wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji madini mbalimbali kanda ya ziwa ikiwemo gesi asilia na mafuta ambalo limeandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali, likiendelea mjini Shinyanga
kongamano la wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji madini mbalimbali kanda ya ziwa ikiwemo gesi asilia na mafuta ambalo limeandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali, likiendelea mjini Shinyanga
kongamano la wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji madini mbalimbali kanda ya ziwa ikiwemo gesi asilia na mafuta ambalo limeandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali, likiendelea mjini Shinyanga
kongamano la wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji madini mbalimbali kanda ya ziwa ikiwemo gesi asilia na mafuta ambalo limeandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali, likiendelea mjini Shinyanga
kongamano la wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji madini mbalimbali kanda ya ziwa ikiwemo gesi asilia na mafuta ambalo limeandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali, likiendelea mjini Shinyanga
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mh. Johari Samizi ambaye ndiye mgeni rasmi katika kongamano la wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji madini mbalimbali kanda ya ziwa ikiwemo gesi asilia na mafuta ambalo limeandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali , akizungumza kwenye ukumbi mjini Shinyanga.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mh. Johari Samizi ambaye ndiye mgeni rasmi katika kongamano la wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji madini mbalimbali kanda ya ziwa ikiwemo gesi asilia na mafuta ambalo limeandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali , akizungumza kwenye ukumbi mjini Shinyanga.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mh. Johari Samizi ambaye ndiye mgeni rasmi katika kongamano la wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji madini mbalimbali kanda ya ziwa ikiwemo gesi asilia na mafuta ambalo limeandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali , akizungumza kwenye ukumbi mjini Shinyanga.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mh. Johari Samizi ambaye ndiye mgeni rasmi katika kongamano la wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji madini mbalimbali kanda ya ziwa ikiwemo gesi asilia na mafuta ambalo limeandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali , akizungumza kwenye ukumbi mjini Shinyanga.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mh. Johari Samizi ambaye ndiye mgeni rasmi katika kongamano la wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji madini mbalimbali kanda ya ziwa ikiwemo gesi asilia na mafuta ambalo limeandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali , akizungumza kwenye ukumbi mjini Shinyanga.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mh. Johari Samizi ambaye ndiye mgeni rasmi katika kongamano la wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji madini mbalimbali kanda ya ziwa ikiwemo gesi asilia na mafuta ambalo limeandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali , akizungumza kwenye ukumbi mjini Shinyanga.
kongamano la wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji madini mbalimbali kanda ya ziwa ikiwemo gesi asilia na mafuta ambalo limeandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali , likiendelea mjini Shinyanga.
kongamano la wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji madini mbalimbali kanda ya ziwa ikiwemo gesi asilia na mafuta ambalo limeandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali , likiendelea mjini Shinyanga.
kongamano la wanawake wanaofanya shughuli ya uchimbaji madini mbalimbali kanda ya ziwa ikiwemo gesi asilia na mafuta ambalo limeandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali , likiendelea mjini Shinyanga.
Social Plugin