Shirika lisilo la
kiserikali linaloitwa ANNA SCHUBERT
MACKEJA KWOFIE Foundation ASMK limetoa msaada wa Saruji na Magudulia 140
yatakayotumiwa na wanafunzi kwa ajili ya kufuata na kuhifadhi maji
Shirika hilo limetoa
magudulia hayo kwa lengo la kuwaondolea usumbufu wanafunzi kutoka na ndoo
nyumbani kwa ajili ya kufuata maji kwenye vyanzo vinavyopatikana umbali mrefu
kutoka katika eneo la shule.
Akizungumza katika hafla
ya kukabidhi msaada huo, Mratibu wa
utemi wa Busiya Mzee Alfred Muyanga amesisitiza
Walimu na wanafunzi kuyatunza magudulia hayo ambayo yatasaidia kuhifadhi maji
hivyo kutoa fursa kwa wanafunzi kuhudhuria vipindi darasani.
Kwa upande wake Mkuu wa
shule ya sekondari Busiya Mwalimu Badi Iddi
Mfinanda amepongeza na kusema msaada huo utasaidia kupunguza changamoto
zilizopo.
Nao baadhi ya wanafunzi
wa shule ya sekondari Busiya wamelishukuru shirika la ASMK kwa kutoa msaada huo
ambao utasaidia kupunguza changamoto zao.
Aidha afisa Elimu wa kata ya Itilima akizungumza kwa niaba ya afisa elimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Renatus Malima amelipongeza na kulishukuru shirika la ASMK kwa kutoa msaada wa magudulia 140 na saruji katika shule ya sekondari Busiya ambapo amewaomba kuendelea na majitoleo hayo kwa lengo la kuisaidia serikali kutatua changamoto zilizopo.
ANNA SCHUBERT MACKEJA KWOFIE ASMK Foundation ni shirika lisilo la kiserikali linalojihusisha na utekelezaji wa miradi mbalimbali katika sekta za elimu na maji Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga,ambalo lipo chini ya himaya ya utemi wa Busiya wa Mtemi Edward Kidaha Makwaia.
Social Plugin