MAGARI, PIKIPIKI LESENI NA VYETI VYA MADEREVA WOTE KUKAGULIWA – RTO LUKOLOLO WANAOPUUZA KUSHURUTISHWA SHINYANGA

 Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Mkuu wa jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani Mkoa wa Shinyanga Mrakibu msaidizi wa Polisi  Debora Lukololo amewataka watumiaji wa vyombo vya moto pamoja na watembea kwa miguu kushiriki kikamilifu maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama.

Amesema jeshi hilo katika wiki ya nenda kwa usalama barabarani  pamoja na shughuli mbalimbali zitakazofanyika litatoa elimu ya usalama barabarani, ukaguzi wa vyombo vya moto  na ukaguzi wa leseni.

Amewataka wananchi kutumia fursa hiyo ili kuzijua sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani ili kuepukana na ajali barabarani

Wakati huo huo mrakibu msaidizi wa Polisi Debora Lukololo amekemea kitendo cha kuhujumu miundombinu ya barabarani ikiwemo alama za usalama barabarani kwani kitendo hicho ni kinyume cha sheria za Nchi.

Machi 13 hadi 17 Mwaka huu 2023 Mkoa wa Shinyanga utaadhimisha wiki ya nenda kwa usalama barabarani na kwamba kauli mbio ya Mwaka huu 2023 inasema ‘TANZANIA BILA AJALI INAWEZAKENA TIMIZA WAJIBU WAKO’