MWALIMU RASHID ATAKA WAZAZI KUFUATILIA MAENDELEO YA WATOTO WAO SHULENI – MWADUI MJINI SHINYANGA

Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Wazazi na walezi wa wanafunzi katika shule ya msingi Mwadui kata ya Ngokolo Manispaa ya Shinyanga wamekumbusha kutimiza wajibu wao kwa watoto ikiwemo malezi bora pamoja na kufuatilia maendeleo ya wanafunzi shuleni.

Wito huo umetolewa na Mwalimu mkuu msaidizi wa shule ya msingi Mwadui, Twaha Rashid wakati akizungumza na Misalaba Blog ambapo pamoja na mambo mengine  amewasisitiza wazazi kuwajibika ipasavyo suala la malezi ili kukomesha vitendo viovu vinavyochangiwa na mmomonyoko wa maadili.

Mwalimu Rashid amesema jamii inawajibu mkubwa wa kufuatilia mienendo ya watoto wao kwa kushirikiana na uongozi wa shule pamoja na serikali za mitaa ili kumlinda mtoto.

Mwalimu Rashid amewaomba wazazi na walezi kuwa mfano kwa watoto wao na kwamba wanapaswa kuishi maisha ambayo yatamjenga na kumuimarisha mtoto katika maisha ya kila siku.