SERIKALI KWA KUSHIRIKIANA NA WALENGWA WA TASAF WAPANDA MITI 1200 MTAA WA DOME - SHINYANGA

Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kwa kushirikiana na walengwa wa kaya maskini unaotekelezwa na mfuko wa maendeleo ya jamii TASAF, wameendelea na zoezi la kupanda miti ikiwa ni hatua ya kutunza mazingira ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi

zoezi hilo leo limefanyika katika Mtaa wa Dome kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga ambapo takribani miche ya miti 1200 imepandwa katika eneo lililopo karibu na ofisi ya serikali ya mtaa huo.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo Afisa Maliasili na Mazingira wa Manispaa ya Shinyanga Bwana Ezra Manjerenga amesema zoezi hilo linatekelezwa chini ya Mradi wa TASAF kwa ajili ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

“Tunaendelea na juhudi zetu kubwa za kutekeleza kampeni ya usimamizi wa mazingira na kwa Manispaa ya Shinyanga tunakampeni inaitwa ‘MTU NA MTI’ lakini vilevile tunatekeleza maagizo ya kila Halmashauri kupanda miti Milion moja na laki tano Shinyanga toka kipindi cha nyuma kwa historia sisi ni wahanga wa mabadiliko ya tabianchi”.amesema afisa mazingira  Manjerenga

“Katika mradi tulionao huu hapa mtaa wa Dome tumepanda miti 1200 na hii inagusa lengo letu la Halmashauri ambapo tunaenda kufikia asilimia 86 sasa ya utekelezaji wa agizo la serikali kwa kila Halmashauri kupanda miti Milion moja na laki tano”.amesema Afisa mazingira Manjerenga  

Manjerenga amesema mbali na mafanikio yaliyopo kupitia lakini pia zoezi hilo limekuwa likikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ufugaji holela hali inayosababisha uharibifu wa miti iliyopandwa.

Aidha Afisa Mazingira  Manjerenga amewaomba wakazi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kujitokeza kwa wingi kufuata miche ya miti inayotolewa bure katika ofisi hiyo ili kupendezesha mazingira.

Mwenyekiti wa mtaa wa Dome Bwana Solomon Nalinga Najulwa amesema atahakikisha mradi huo anausimamia ipasavyo ili  kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Katika zoezi hilo Mzabuni na mshauri wa kamati ya TASAF mtaa wa Dome Joseph Kisanko amesema kuwa lengo la mradi huo ni kuboresha mazingira.

Nao baadhi ya walengwa wa TASAF ambao wanatekeleza mradi huo wa upandaji miti wamesema pamoja na faida nyingine lakini pia kupitia mradi huo wanajikwamua kiuchumi kupitia ujira wanaolipwa

Shughuli hiyo imehudhuriwa na wananchi, wadau, viongozi wa serikali pamoja na viongozi wa chama ambapo nao wamesisitiza juu ya ushirikiano katika kutunza mazingira.

Afisa Mariasili na Mazingira wa Manispaa ya Shinyanga Bwana Ezra Manjerenga akitoa elimu kuhusu namna bora ya upandaji wa miti.

Afisa Mariasili na Mazingira wa Manispaa ya Shinyanga Bwana Ezra Manjerenga akitoa elimu kuhusu namna bora ya upandaji wa miti.

Upande wa kushoto ni Mzabuni na mshauri wa kamati ya TASAF mtaa wa Dome Joseph Joaster Kasanko na upande wa kulia ni Mwenyekiti wa mtaa wa Dome Bwana Solomon Nalinga Najulwa wakishiriki katika zoezi la kupanda miti.Upande wa kushoto ni Mzabuni na mshauri wa kamati ya TASAF mtaa wa Dome Joseph Joaster Kasanko na upande wa kulia ni Mwenyekiti wa mtaa wa Dome Bwana Solomon Nalinga Najulwa wakishiriki katika zoezi la kupanda miti.