Mkuu wa Wilaya ya
Shinyanga Mh. Johari Samizi amesema serikali itawachukulia hatua wazazi na
walezi wa watoto waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza Mwaka wa masomo
2023 ambao mpaka sasa hawajaripoti shuleni bila sababu za msingi.
Ameyasema hayo leo
wakati akizungumza na Misalaba Blog ofisini kwake ambapo amesema mpaka sasa ni
asilimia 91 ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika
Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga wameripoti shuleni, wakati asilimia 80
katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga wameanza masomo.
DC Samizi ametumia
nafasi hiyo kuendelea kuwakumbusha wazazi kuhakikisha watoto wote
waliochaguliwa wanaripoti shuleni ili waweze kuendelea na masomo kama
ilivyoelekezwa na serikali.
“Mpaka
jana Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga tayari wameripoti asilimia 91 kuna
asilimia 9 ya watoto bado hawajaripoti shule lakini katika Halmashauri ya
Shinyanga vijijini mpaka jana walioripoti ni asilimia 80 kwahiyo kuna asilimia
20 bado hawajaripoti shule lakini serikali ya Mkoa wa Shinyanga imeshatoa
maelekezo kwamba hata kama mtoto hana sale mtoto huyo aende shule ili aweze
kupata masomo kama wengine”.
Kwahiyo
rai yangu ni kwamba wazazi wote ambao watoto wao wamechaguliwa kujiunga na
kidato cha kwanza wahakikishe kufikia jumatatu wiki ijayo watoto hao wawe wamekwenda
shule na wanavyozidi kukaa na watoto hao hatua kali zitachukuliwa dhidi yao na
sisi tunavyowapa huu muda siyo kwamba hatufuatilii tunatakwimu tunafahamu nani
alichaguliwa na nani alikwenda shule ya kulipia”.amesema
DC Samizi
Mkuu huyo wa Wilaya ya Shinyanga Mh. Johari Samizi amesema serikali inaendelea na juhudi mbalimbali za kuhakikisha wanafunzi hao wanaripoti shuleni wakati wazazi na walezi wakiendelea kukamilisha mahitaji muhimu ya watoto hao ikiwemo sale za shule na vitu vingine.
Social Plugin