Na Mapuli Misalaba, Shinyanga
Mkuu wa Wilaya ya
Shinyanga Mh. Johari Samizi ametoa wito kwa wananchi wote wa Wilaya ya
Shinyanga, kununua mahindi yanayouzwa na serikali kwa bei nafuu, ili kukabiliana
na mfumko wa bei unaosababishwa na sababu mbalimbali ikiwemo mtikisiko wa
kiuchumi.
DC Samizi ameyasema
hayo leo wakati wa mahojiano maalum na Misalaba Blog ambapo amesema mahindi
hayo, yametolewa na serikali kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula NFRA
ili kuwauzia wananchi kwa bei nafuu ya shilingi Mia nane hamsini (850) badala
ya shilingi elfu moja mia tano (1500) bei ya sokoni.
Mkuu huyo wa Wilaya ya
Shinyanga Mh. Johari Samizi amesema lengo la serikali ni kupunguza ukali wa
maisha kwa wananchi wake unaotokana na sababu mbalimbali ikiwemo mtikisiko wa
kiuchumi, na ukame uliosababishwa na mabadiliko ya tabia Nchi,
“Mahindi
hayo yametolewa na serikali kupitia ghara la Taifa NFRA na kama mnavyofahamu
kwa upande huu wa kanda ya ziwa ghara kuu la NFRA lipo katika Mkoa wetu huu wa Shinyanga lakini
mmeweza kusikia kuna malalamiko ya mfumko wa bei ya chakula lakini pia mmeona
hali ya mabadiliko ya tabia Nchi yameathiri swala zima la kilimo”.
“kwahiyo
ili kukabiliana na mfumko wa bei serikali ikaona sasa kuwapunguzia wananchi
wake ukali wa maisha kwa sababu mahindi hayo kwa bei ya sokoni yanaunzwa
kuanzia bei ya 1200 hadi 1500 lakini kupitia mahindi haya ambayo yametolewa na
serikali yanauzwa kilo moja kwa bei ya 8500”.amesema DC
Samizi
Amewataka wenyeviti wa mtaa pamoja na watendaji
Wilayani Shinyanga kusimamia zoezi hilo
kwa uaminifu na uadilifu ikiwa ni pamoja na kuzingatia bei elekezi ili wananchi
waweze kufaidika na fursa hiyo.
Aidha DC Samizi amewaomba wananchi kutumia fursa hiyo kununua mahindi yaliyotolewa na serikali kwa bei nafuu,ambapo ameonya mahindi hayo yatumike kwa chakula na kwamba yasibadilishiwe matumizi.
Social Plugin