Na Mapuli Misalaba, Shinyanga
Waandishi wa habari za mtandaoni Nchini wametakiwa
kuzingaia sheria zilizopo katika sekta hiyo na kwamba wanapaswa kuandika habari zenye kuleta matokeo chanya kwa
wananchi na serikali kwa jumla.
Hayo yamezungumza na mkurugenzi wa idara ya habari
Maelezo na msemaji mkuu wa serikali Gerson Msigwa akiwa mgeni rasmi kwenye hafla
ya uzinduzi wa taasisi ya waandishi wa habari mtandaoni (Tanzania Online Media
Alliance) TOMA iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mwl. Julius Nyerere
uliopo katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
Hafla hiyo imeratibiwa na chama cha waandishi wa
habari Mkoa wa Arusha (APC) kwa
ufadhili wa Mfuko wa Maendeleo wa Watu wa Marekani kupitia taasisi za Freedom
House pamoja na PACT ambapo Msingwa amewasisitiza waandishi hao kuzingatia maadili
yao.
Mkurugenzi
wa idara ya habari Maelezo na msemaji mkuu wa serikali Gerson Msigwa akiwa
amemwakilishi waziri wa habari, mawasiliano na teknolojia ya habari Mh. Nape
Nnauye, ametumia nafasi hiyo kuwataka waandishi wa habari za mtandaoni kuandika
habari kwa weledi na kuepuka habari za upotoshaji ambazo huzua taharuki na
huchochea mgogoro Nchini.
“Tasnia ya habari
iko mikononi mwa vyombo vya habari mtandaoni, twendeni tukaoneshe weledi wa
hali ya juu hicho ndicho kitakachotufanya tuaminike na jamii lakini pia ni
lazima tuangalie maadili ya uandishi wa habari yanasema nini, ni lazima
tuangalie sheria za Nchi yetu zinasema nini hatuwezi kuwa waandishi wa habari
za mtandaoni kwa kujikita tu kwenye kuzua taharuki, kuvunja sheria au
kuchonganisha jamii na jamii au jamii na serikali”.amesema Msigwa
“Tumetoka tulipotoka vyombo vya habari vikimilikiwa na wanasiasa na wafanyabiashara, akija mmiliki anasema weka hiki usiweke hiki. Tuacheni kutumika, hapo ndipo heshima yetu itakuwepo, fanya kazi yako kwa weledi”.amesema Msigwa
Aidha Msigwa amewasisitiza waandishi wa habari wenye elimu ya chini kujiendeleza ili kuimarika zaidi huku akipongeza juhudi za chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Arusha (APC) kwa kuanzisha wazo hilo ambapo itasaidia waandishi wa habari za mtandaoni waweze kuwa na weledi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.
Katika taarifa yake Mwenyekiti wa chama cha
waandishi wa habari Mkoa wa Arusha Bwana Claud Gwandu amesema TOMA imeanzishwa
baada ya chama hicho APC kumaliza mradi
waliokuwa wakitekeleza wenye lengo la kusaidia waandishi wa habari za mtandaoni
ambao walikuwa na changamoto mbalimbali za kitaaluma ambapo mafunzo ya aina
mbalimbali yalitolewa ili kuwaimarisha na kupunguza tatizo la ajira kwa
waandishi wa habari.
“Toma
imesajiliwa rasmi Mwaka jana 2022 baada ya mradi uliokuwa unaendeshwa na Arusha
Press Club (APC) kwa kushirikiana na Freedom House pamoja na PACT mradi
huu ulianza Mwaka 2018 na ulikuwa na malengo ya kuwasaidia waandishi wa habari
za mtandaoni ambao walikuwa na changamoto mbalimbali za kitaaluma mwanzoni
tulianza na waandishi wa habari za mtandaoni 23 kutoka mikoa mbalimbali ya hapa
Tanzania”. amesema
Mwenyekiti wa APC Gwandu
“Katika utekelezaji wa mradi huo
tulikuwa tukitoa mafunzo ya aina mbalimbali ikiwemo mafunzo ya kiusalama
kazini, mafunzo ya sheria za uandishi wa habari, mafunzo kuhusu maadili na
kanuni za uandishi wa habari na mambo mengine mbalimbali”. amesema Gwandu
“Baada ya kuelekeza kumaliza mradi huo tukaona kwamba kuna unaumuhimu wa kuanzisha chombo ambacho kitakuwa kinasimamia yale ambayo yalikuwa yanafanywa na Club ya waandishi wa habari Mkoa wa Arusha katika kutekeleza mradi na hiki chombo kiko wazi kwa waandishi wa habari wa Tanzania nzima wanaojihusisha na uandishi wa habari za mtandaoni ambao wanauhiari wa kujiunga na chombo hiki”.amesema Mwenyekiti wa APC Gwandu
Baadhi ya wadau mbalimbali waliohudhuria uzinduzi huo wamekipongeza chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Arusha kwa kuanzisha wazo hilo ambapo wameahidi kuendeleza kushirikiana na TOMA huku wakiwaomba waandishi wa habari za mitandaoni kutumia fursa hiyo ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Kwa upande wake makamu Mwenyekiti wa Tanzania Online
Media Alliance (TOMA), Salome Kitomari amesema atahakikisha taasisi hiyo inafanya
kazi kwa mujibu wa taaluma huku akiwakumbusha waandishi wa habari kutumia fursa
hiyo ikiwa ni pamoja na kuweka maudhui mazuri.
Makamu Mwenyekiti wa TOMA ambaye nia ni Mwenyekiti taasisi ya vyombo vya
habari kusini mwa Afrika tawi la Tanzania (MISA TANZANIA) Salome Kitomari
ametumia nafasi hiyo kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia
Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anazofanya katika kuimarisha umoja wa Taifa huku
akiishukuru serikali kwa kuweka uhuru wa vyombo vya habari.
Hafla ya uzinduzi wa taasisi ya waandishi wa habari
mtandaoni (Tanzania Online Media Alliance) TOMA imeratibiwa na chama cha
waandishi wa habari Mkoa wa Arusha (APC) kwa ufadhili wa Mfuko wa Maendeleo wa Watu wa Marekani
kupitia taasisi za Freedom House pamoja na PACT.
Uzinduzi
huo umehudhuriwa na wadau mbalimbali wa habari akiwemo Mkurugenzi wa Tanzania Media Foundation (TMF) Dastan
Kamanzi, Mkurugenzi wa Freedom House Daniel Mahal Lema, Mwenyekiti taasisi ya
vyombo vya habari kusini mwa Afrika tawi la Tanzania (MISA TANZANIA) Salome
Kitomari, Mtaalam wa mambo ya habari kutoka ubalozi wa Marekani Japhet Sanga
akiwa amemwakilisha kaimu mkurugenzi wa USAID, Bwana Bret Saalwaechter.
Wadau
wengine waliohudhuria uzinduzi huo ni pamoja na mwakilishi wa Legal and Human
Rights Centre (LHRC) Hidaya Haonga, Mwakilishi wa Tanzania media coomen’s Association (TAMWA) Bwana Godwin Assenga
pamoja na Mwakilishi wa MISA TAN Tanzania Bwana Augustino Lucas.
Aidha waandishi wa habari kutoka katika vyombo vya habari ikiwemo Blogs na Online Tv kutoka mikoa mbalimbali Nchini Tanzania wameshiriki uzinduzi huo wa taasisi huo wa taasisi ya waandishi wa habari mtandaoni (Tanzania Online Media Alliance) TOMA ambao umefanyika Ijumaa Februari 10,2023 na kwamba umeratibiwa na chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Arusha (APC) kwa ufadhili wa Mfuko wa Maendeleo wa Watu wa Marekani kupitia taasisi za Freedom House pamoja na PACT.
Mgeni rasmi wa pili kutoka upande wa kushoto mkurugenzi wa idara ya habari Maelezo na msemaji mkuu wa serikali Gerson Msigwa awali akiingia ukumbini kwa ajili ya uzinduzi rasmi wa TOMA.
Akipokelewa Mgeni rasmi wa pili kutoka upande wa kushoto mkurugenzi wa idara ya habari Maelezo na msemaji mkuu wa serikali Gerson Msigwa awali akiingia ukumbini kwa ajili ya uzinduzi rasmi wa TOMA.

Mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Arusha Bwana Claud Gwandu akisoma taarifa fupi ya kuanzishwa kwa Taasisi ya waandishi wa habari mtandaoni (TOMA).

Mkurugenzi wa idara ya habari Maelezo na msemaji mkuu wa serikali Gerson Msigwa akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa taasisi ya waandishi wa habari mtandaoni uliofanyika katika ukumbi wa Morena Hotel jijini Dodoma.
Makamu mwenyekiti wa Taasisi ya waandishi wa habari mtandaoni (TOMA) ambaye pia ni Mwenyekiti taasisi ya vyombo vya habari kusini mwa Afrika tawi la Tanzania (MISA TANZANIA) Salome Kitomari akizungumza kwenye uzinduzi wa Tanzania Online Media Alliance (TOMA).
Mtaalam wa mambo ya habari kutoka ubalozi wa Marekani Japhet Sanga akiwa amemwakilisha kaimu mkurugenzi wa USAID, Bwana Bret Saalwaechter akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa TOMA.

Mtaalam wa mambo ya habari kutoka ubalozi wa Marekani Japhet Sanga akiwa amemwakilisha kaimu mkurugenzi wa USAID, Bwana Bret Saalwaechter akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa TOMA.
Hafla ya uzinduzi wa taasisi ya waandishi wa habari mtandaoni ikiendelea katika ukumbi wa Mwl. Julius Nyerere uliopo katika Hotel ya Morena jijini Dodoma.
Hafla ya uzinduzi wa taasisi ya waandishi wa habari mtandaoni ikiendelea katika ukumbi wa Mwl. Julius Nyerere uliopo katika Hotel ya Morena jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa idara ya habari Maelezo na msemaji mkuu wa serikali Gerson Msigwa akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa taasisi ya waandishi wa habari mtandaoni uliofanyika katika ukumbi wa Morena Hotel jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa idara ya habari Maelezo na msemaji mkuu wa serikali Gerson Msigwa akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa taasisi ya waandishi wa habari mtandaoni uliofanyika katika ukumbi wa Morena Hotel jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa idara ya habari Maelezo na msemaji mkuu wa serikali Gerson Msigwa akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa taasisi ya waandishi wa habari mtandaoni uliofanyika katika ukumbi wa Morena Hotel jijini Dodoma.
(Tanzania Online Media Alliance) TOMA Seif Mangwangi akizungumza katika hafla hiyo ya uzinduzi wa TOMA
.
Mkurugenzi wa idara ya habari Maelezo na msemaji mkuu wa serikali Gerson Msigwa akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa taasisi ya waandishi wa habari mtandaoni uliofanyika katika ukumbi wa Morena Hotel jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa idara ya habari Maelezo na msemaji mkuu wa serikali Gerson Msigwa akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa taasisi ya waandishi wa habari mtandaoni uliofanyika katika ukumbi wa Morena Hotel jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa idara ya habari Maelezo na msemaji mkuu wa serikali Gerson Msigwa akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa taasisi ya waandishi wa habari mtandaoni uliofanyika katika ukumbi wa Morena Hotel jijini Dodoma.


Social Plugin