KAMATI YA SIASA YA CCM WILAYA YA SHINYANGA MJINI YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI MANISPAA YA SHINYANGA YAPONGEZWA KWA UTEKELEZAJI WA ILANI

Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Kamati ya siasa ya chama cha mapinduzi CCM Wilaya ya Shinyanga mjini, Februari 17, 2023 imefanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayoondelea kutekelezwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga ikiwemo ujenzi wa soko kuu la kisasa mjini Shinyanga.

Akizungumza Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga mjini Anord Makombe ametumia nafasi hiyo kupongeza juhudi mbalimbali zinazofanywa na serikali katika utatuzi wa changamoto za wananchi Manispaa ya Shinyanga.

“Niipongeze Manispaa yetu ya Shinyanga chini ya Mstahiki Meya lakini pia na Mkurugenzi wetu na wataalam wetu kwa juhudi za maksudi zinazofanywa tunauona mji wetu unavyobadilika na tunaamini kabisa kwamba unaenda kutuongezea hadhi badaye”.amesema Mwenyekiti Makombe

Katika ziara hiyo  Misalaba Blog imezungumza na mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mh. Johari Samizi ambaye amewasisitiza wataalam na wakuu wa idara  wa Halmashauri ya Manispaa wanaosimamia miradi kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati ili wananchi waweze kunufaika.

DC Samizi amewaomba wananchi wa Wilaya ya Shinyanga kuendelaa kuunga mkono juhudi za serikali ambapo amesema atasimamia kuhakikisha miradi inawanufaisha wananchi kama mpango wa serikali chini ya ilani za chama cha mapinduzi CCM.

Aidha Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mh. Johari Samizi ametumia nafasi hiyo kuendelea kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha za miradi kwa lengo la kutatua changamoto zinazowakabili  wakazi wa Wilaya hiyo ya Shinyanga.

Misalaba Blog pia imezungumza na katibu wa itikadi, siasa na uenezi wa CCM Wilaya ya Shinyanga mjini Bwana Said Bwanga ambaye  ametaja baadhi ya maeneo ambayo kamati ya siasa  imetembelea na kukagua huku akitaja maagizo  yaliyotolewa na kamati hiyo.

“Katika ziara yetu tumetembelea shule ya wasichana iliyopo Butengwa kata ya Ndembezi katika shule hiyo tumeona maendeleo yanakwenda vizuri na mpaka sasa hatua iliyofikiwa ni hatua kubwa tumeambia ni takribani asilimia 80 vilevile tumeweza kutembelea zahanati ya Seseko na ujenzi wa barabara ya Seseko kwa kweli serikali hii inayoongozwa na Rais mama yetu Dkt. Samia Suluhu Hassan wanafanya vizuri daraja la Ndembezi limejengwa vizuri tena kwa kiwango wa juu”.

“Tumetembelea daraja la Old Shinyanga nalo uongozi wa Manispaa ya Shinyanga wameliboresha vizuri hakuna kero tena kwa wananchi tulipotoka pale tumetembelea mradi wa maji kata ya Chibe kwa kweli tumeona mradi unaendelea vizuri, tumetembelea ujenzi wa kituo cha Afya Kambarage hatujabaini changamoto”.amesema Bwanga

“Kamati ya siasa tumeweza kutembelea ujenzi wa soko la wamachinga lililopo Ngokolo ambapo tumeomba mnada unaofanyika Jumamosi tu uwe unafanyika siku mbili Jumamosi na Jumapili lakini pia wawekewe taa ili wananchi waweze kufanyakazi mpaka usiku lakini tumeenda kutembelea soko kuu la mjini tumeona ujenzi unaendelea vizuri”.

“Kamati ya siasa pia tumetembelea eneo la Lubaga katika ujenzi wa barabara inayotokea Lubaga kuelekea Old Shinyanga pamoja na kwamba mkandarasi alikuwa amepewa miezi kumi awe amemaliza ambayo bado haijaisha lakini katika vile vifusi imekuwa ni kero na changamoto kwa wananchi wa Shinyanga mara nyingi ajali zinatokea pale kwahiyo chama cha mapinduzi kimetoa maagizo mkandarasi kuanzi sasa awe anamwagia maji katika maeneo hayo kuzuia vumbi wakati wakiendelea na ukarabati wakati huo huo tumewaagiza wakamilishe haraka tuta lililopo barabarani lisije kuleta ajali”.amesema Katibu Mwenezi Bwanga

Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Shinyanga Mjini Naibu Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu kazi,vijana, ajira  na wenye ulemavu,Paschal Patrobas amesema hatua mbalimbali za uboreshaji wa masoko zinaendelea vizuri  katika jimbo hilo.

Kamati ya siasa ya CCM Wilaya ya Shinyanga mjini imetembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika kata ya Ndembezi, Old Shinyanga, Chibe, Kambarage, Ngokolo pamoja na kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga, ikiwa ni hatua ya kusimamia ilani ya chama hicho.