
Wanawake wametakiwa
kuchangamkia mikopo yenye riba nafuu inayotolewa na Halmashauri badala ya
kuchukua mikopo kandamiza ambayo imekuwa ikiwasababishia migogoro na kufilisiwa
mali.
Rai hiyo imetolewa na
Mwenyekiti wa Mtaa wa Dome kata ya Ndembezi Bwana Solomon Nalinga wakati
akizungumza na Wanawake wa Mtaa huo kwenye kikao kilicholenga kubainisha fursa
mbalimbali zilizopo kwa kundi hilo.
Bwana Nalinga amewaomba
wanawake wa mtaa huo kujiunga kwenye vikundi
kama moja ya sifa na vigezo vya kupata mikopo inayotolewa na halmashauri
kwa riba nafuu
Misalaba Blog
imezungumza na baadhi ya wanawake wa mtaa wa Dome waliohudhuria kikao hicho
ambapo wameahidi kuwa mabalozi waaminifu kwa wanawake wengine wanaojiunga
kwenye vikundi kwa ajili ya kuchukua mikopo.
Social Plugin